Msangi umekuwa kamanda anayechagua pori?
Ni hivi tu, aaaa anyway
natumai watu wote mu wazima wa afya na mnaendelea na majukumu yenu ya kikazi hasa katika dunia hii iliyojaa mbwembwe, majigambo, kujisifu na hata aaa yaani hali ya watwawala wetu aa sorry naamanisha watawala wetu wanavyotulaghai kwa maneno mataam na si wenyewe tunakubali tu si tumezoea.
Nasema haya nikikumbuka tukio lililotokea mapema mwezi huu huko wilayani Mbozi katika mji mdogo wa Tunduma ambao unakuwa kwa kasi katika masuala ya kibiashara.
Kwa wasioifahamu wilaya ya Mbozi ina vijisifa kiasi, ingawa havipendezi masikioni, kwa mfano uchunaji wa ngozi za binadamu pamoja na utangenezaji wa silaha haramu maarufu kama magobole ambayo yanatumika katika uhalifu hawa jamaa ni stadi kwa hilo, sasa sijuin kwanini utaalamu wao wa kutengeneza silaha hauboreshwi, lakini hilo la ngozi inafaa lilaaniwe kwa nguvu zote.
Katika tukio la Tunduma, mtanzania mmoja aliyejulikana kwa jina Lucas Msuya alimaarufu mangi aliuawa kwa kupigwa na polisi wa Zambia kwa kile alichodaiwa kuwa ni kununua mali za wizi.
Kama kawaida vyombo vya habari vya ndani na nje vilihamasika kwa kiasi kikubwa kuipata habari hiyo kwa kuwa ilikuwa ni ishu ya kimataifa.
Kwa hili sitasita kuwapongeza waandishi wa habari Mkoa wa Mbeya kwa jinsi walivyojitahidi kufuatilia na kuripoti matukio yote yaliyokuwa yanatokea huko na kuwafanya watanzania wote wawe makini na kujua hali halisi ya kinachojiri Mkoani Mbeya hususani katika mji wa Tunduma.
Ngoja niwapongeze hawa walifanya kazi kubwa kweli kweli, Ramandani msangi, Rashid Mkwinda,solomoni Mwansele aaa ni wengi hao ni kwa uchache kwa kweli walifanya kazi nzuri.
Haikuishia hapo bwana msangi akapandisha habari yake nzuri kabisa katika blog, ikieleza jinsi mkuu wa kaya ya Mbeya alivyokuwa akiongea na wakazi wa tunduma kuelezea kile alichoongea na maafisa wa serikali ya zambia.
Ilidaiwa kuwa Mkuu huyo wa kaya ya Mbeya,Tunduma ikiwa ndani yake alitamba kuwa watanzania wamechoka kunyanyaswa, akasema zaidi kuwa serikali ya zambia imekiri kuhusika na mauaji hayo na tamu zaidi ni kwamba imeundwa tume itakayochunguza chanzo cha vurugu hizo pamoja na timu ya Madaktari wa tanzania na Zambia wataoufanyia uchunguzi mwili wa marehemu msuya au mangi.
Akaja naye Mkuu wa polisi, huyu alijifaragua kuwa hawatavumilia kuona watanzania wananyanyaswa wakiwa ndani ya nchi yao na nje ya nchi,huku akiwata wananchi watulize mzuka na kuiachia serikali ichukua hatua zaidi kuhusiana na suala hilo.
Kweli waandishi hao baadhi niliwataja na wengine walifanya kazi kubwa kuufahamisha umma wa tanzania tangu mwanzo wa tukio hadi kauli hizo zao wanaotungoza kwa kasi kuelekea maisha, ambayo tunaambiwa ni bora huku matatizo yakiongezeka kila kukicha hususani umeme, lakini nasikia mwezi octoba kuna mvua ya kutengeneza itaanza kunyesha kwa malipo ya tushilingi milioni mbili, Waziri Mkuu amesema eti hizo ni hela kidogo tu, mi sina hakika kama ni kweli.
Aaaa tuyaache hayo, lakini ikiwa ni takribani wiki mbili sasa nilikuwa nasubiri baada ya Msangi na timu ya wenzake kingefuata nini naona wapo kimya, sidhani kama ndio habari ya Tunduma wameachana nayo, aaa sijasema hivyo labda wanatafakari waanze vipi, sidhani kama wanataka watoke vipi maana walikwisha toka.
Labda wakati wanatafakari wajaribu kuyaona haya, hivi familia ya mangi imelipwa fidia gani kutokana na mauaji hayo ya makusudi, lakini bado najiuliza huku nikiwa na shaka shaka moyoni, inadaiwa marehemu huyu alikabidhiwa na polisi wa tanzania kwa polisi wa Zambia ambao baadae walitoa kipigo kikali na kusababisha kifo cha kijana huyu ambaye ni nguvu kazi ya Taifa loo masikini natumai bado taifa lilikuwa linamuhitaji.
Nilisikia polisi wawili wa Zambia wanaodaiwa kusababisha kifo hicho hicho walitiwa korokoroni na baadae kufikishwa mahakamani, sasa sijajua nini hatma ya wale askari walimuweka chambo kijana huyo kushindwa kufuatilia kujua nini kinampata kijana huyo wa Kitanzania ambaye ni mwenzao tatizo ni moja tu hakuwa askari labda ndio maana walimsahau.
Pamoja na hayo hiyo ripoti sijajua inangoja nini, Msangi, Mkwinda na wengine waandishi mliopo Mbeya vipi mbona kimya tulitaraji kuona mfululizo wa habari za tunduma ili nasi tukae huku tukiwa tumejibweda na kumwaga stori za tunduma kana kwamba tupo tunashuhudia kumbe nyie mnacheza heko ya kutuhabarisha.
Msilale tupeni mambo au Mmekuwa makamanda wanaochagua pori???
Sitaki kuamini hilo
tchao
natumai watu wote mu wazima wa afya na mnaendelea na majukumu yenu ya kikazi hasa katika dunia hii iliyojaa mbwembwe, majigambo, kujisifu na hata aaa yaani hali ya watwawala wetu aa sorry naamanisha watawala wetu wanavyotulaghai kwa maneno mataam na si wenyewe tunakubali tu si tumezoea.
Nasema haya nikikumbuka tukio lililotokea mapema mwezi huu huko wilayani Mbozi katika mji mdogo wa Tunduma ambao unakuwa kwa kasi katika masuala ya kibiashara.
Kwa wasioifahamu wilaya ya Mbozi ina vijisifa kiasi, ingawa havipendezi masikioni, kwa mfano uchunaji wa ngozi za binadamu pamoja na utangenezaji wa silaha haramu maarufu kama magobole ambayo yanatumika katika uhalifu hawa jamaa ni stadi kwa hilo, sasa sijuin kwanini utaalamu wao wa kutengeneza silaha hauboreshwi, lakini hilo la ngozi inafaa lilaaniwe kwa nguvu zote.
Katika tukio la Tunduma, mtanzania mmoja aliyejulikana kwa jina Lucas Msuya alimaarufu mangi aliuawa kwa kupigwa na polisi wa Zambia kwa kile alichodaiwa kuwa ni kununua mali za wizi.
Kama kawaida vyombo vya habari vya ndani na nje vilihamasika kwa kiasi kikubwa kuipata habari hiyo kwa kuwa ilikuwa ni ishu ya kimataifa.
Kwa hili sitasita kuwapongeza waandishi wa habari Mkoa wa Mbeya kwa jinsi walivyojitahidi kufuatilia na kuripoti matukio yote yaliyokuwa yanatokea huko na kuwafanya watanzania wote wawe makini na kujua hali halisi ya kinachojiri Mkoani Mbeya hususani katika mji wa Tunduma.
Ngoja niwapongeze hawa walifanya kazi kubwa kweli kweli, Ramandani msangi, Rashid Mkwinda,solomoni Mwansele aaa ni wengi hao ni kwa uchache kwa kweli walifanya kazi nzuri.
Haikuishia hapo bwana msangi akapandisha habari yake nzuri kabisa katika blog, ikieleza jinsi mkuu wa kaya ya Mbeya alivyokuwa akiongea na wakazi wa tunduma kuelezea kile alichoongea na maafisa wa serikali ya zambia.
Ilidaiwa kuwa Mkuu huyo wa kaya ya Mbeya,Tunduma ikiwa ndani yake alitamba kuwa watanzania wamechoka kunyanyaswa, akasema zaidi kuwa serikali ya zambia imekiri kuhusika na mauaji hayo na tamu zaidi ni kwamba imeundwa tume itakayochunguza chanzo cha vurugu hizo pamoja na timu ya Madaktari wa tanzania na Zambia wataoufanyia uchunguzi mwili wa marehemu msuya au mangi.
Akaja naye Mkuu wa polisi, huyu alijifaragua kuwa hawatavumilia kuona watanzania wananyanyaswa wakiwa ndani ya nchi yao na nje ya nchi,huku akiwata wananchi watulize mzuka na kuiachia serikali ichukua hatua zaidi kuhusiana na suala hilo.
Kweli waandishi hao baadhi niliwataja na wengine walifanya kazi kubwa kuufahamisha umma wa tanzania tangu mwanzo wa tukio hadi kauli hizo zao wanaotungoza kwa kasi kuelekea maisha, ambayo tunaambiwa ni bora huku matatizo yakiongezeka kila kukicha hususani umeme, lakini nasikia mwezi octoba kuna mvua ya kutengeneza itaanza kunyesha kwa malipo ya tushilingi milioni mbili, Waziri Mkuu amesema eti hizo ni hela kidogo tu, mi sina hakika kama ni kweli.
Aaaa tuyaache hayo, lakini ikiwa ni takribani wiki mbili sasa nilikuwa nasubiri baada ya Msangi na timu ya wenzake kingefuata nini naona wapo kimya, sidhani kama ndio habari ya Tunduma wameachana nayo, aaa sijasema hivyo labda wanatafakari waanze vipi, sidhani kama wanataka watoke vipi maana walikwisha toka.
Labda wakati wanatafakari wajaribu kuyaona haya, hivi familia ya mangi imelipwa fidia gani kutokana na mauaji hayo ya makusudi, lakini bado najiuliza huku nikiwa na shaka shaka moyoni, inadaiwa marehemu huyu alikabidhiwa na polisi wa tanzania kwa polisi wa Zambia ambao baadae walitoa kipigo kikali na kusababisha kifo cha kijana huyu ambaye ni nguvu kazi ya Taifa loo masikini natumai bado taifa lilikuwa linamuhitaji.
Nilisikia polisi wawili wa Zambia wanaodaiwa kusababisha kifo hicho hicho walitiwa korokoroni na baadae kufikishwa mahakamani, sasa sijajua nini hatma ya wale askari walimuweka chambo kijana huyo kushindwa kufuatilia kujua nini kinampata kijana huyo wa Kitanzania ambaye ni mwenzao tatizo ni moja tu hakuwa askari labda ndio maana walimsahau.
Pamoja na hayo hiyo ripoti sijajua inangoja nini, Msangi, Mkwinda na wengine waandishi mliopo Mbeya vipi mbona kimya tulitaraji kuona mfululizo wa habari za tunduma ili nasi tukae huku tukiwa tumejibweda na kumwaga stori za tunduma kana kwamba tupo tunashuhudia kumbe nyie mnacheza heko ya kutuhabarisha.
Msilale tupeni mambo au Mmekuwa makamanda wanaochagua pori???
Sitaki kuamini hilo
tchao
